Skip to main content

Mtangazaji Shaffie Weru Ateza Uvumi Uliosambazwa Kuhusu Ajali Yake

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

This archive report was first published on 21 December 2019.

Mtangazaji Shaffie Weru amepinga madai yaliyosambazwa mitandaoni kwamba alihusika kwenye ajali iliyotokea eneo la Northen Bypass.

Kwa mujibu wa picha zilizosambaa mitandaoni, Shaffie anaonekana amesimama kando ya mabaki ya gari la aina ya Mercedes G Wagon, lenye thamani ya mamilioni ya pesa.

Kwenye ukurasa wake wa Twitter, Shaffie alichapisha ujumbe akiwataka mashabiki zake kuwa watulivu kwani alikuwa yuko salama salmini na wala hakuhusika kwenye ajali yoyote.

"Sijahusika kwa ajali yoyote jinsi inavyosemwa. Nilikuwa nimeenda kumsaidia mwathiriwa wa ajali ambaye ni rafiki yangu. Mkiziangalia kwa makini picha zinazosambazwa mitandoani mtaona jinsi ninavyojishughulisha kusaidia pale ninapoweza," Shaffie alisema.

Shaffie alidokeza kwamba rafiki yake huyo ambaye hakumtaja alikuwa akielekea Nairobi kuhudhuria mchezo wa gofu kabla ya gari hilo kugongwa na lori eneo lake la mbele.

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →