This archive report was first published on 17 October 2019.
Bwana harusi aliyeripotiwa kutoweka baada ya kutekwa nyara na watu wasiojulikana Jumatatu Oktoba 7, amepatikana Jumatano Oktoba 16, na asema mipango ya harusi bado ipo.
James Mwamburi alipatikana karibu na eneo la Man Eaters katika barabara ya Mbololo, akiwa amefungwa miguu na mikono.
Alitekwa nyara na watu wasiojulikana Jumatatu Oktoba 7, na familia yake ilimpeleka katika hospitali ya Voi ambapo alifanyiwa ukaguzi wa kimatibabu kabla ya kuruhusiwa kwenda nyumbani.
Alisema mipango ya harusi ingali ipo na itafanyika mwezi Desemba, na kipenzi chake cha Roho Dorcas Wairimu pia ilisema kuwa harusi bado ipo.