This archive report was first published on 16 October 2019.
Wakazi wa Isiolo wamekuwa wakishuhudia uhaba wa maji kwa muda mrefu, na hii inaonekana kuwa inaathiri maisha ya ndoa ya wanaume katika eneo hilo.
Mbunge wa Isiolo Kusini Hassan Odha amedai kuwa wanaume katika eneo lake wameepuka tendo la ndoa kwa ajili ya uhaba wa maji.
Odha alisema hivi siku ya Jumatano Oktoba 16, 2019, akiwa mjini Isiolo, kwamba baadhi ya wanaume wamenilalamikia kwamba hawajakuwa wakishiriki tendo la ndoa kwa miezi kadhaa sasa kwa ajili ya ukosefu wa maji.
Odha alisema, "Baadhi ya wanaume wamenilalamikia kwamba hawajakuwa wakishiriki tendo la ndoa kwa miezi kadhaa sasa kwa ajili ya ukosefu wa maji, maji yamekuwa ghali mno na hata hawafurahii maisha yao ya ndoa."
Idara ya utabiri wa hali ya anga inatangaza kuwa sehemu kadhaa za nchi zitashuhudia mvua kubwa, ambayo inaweza kusababisha kupungua kwa uhaba wa maji.