This archive report was first published on 28 December 2019.
Maafisa wa KWS waliwakamata baada ya kudaiwa kuwaibia jamaa wa familia moja ambao walikuwa wametoka sherehe ya kulipa mahari. Hii ilikuwa baada ya makachero wa Idara ya Upelelezi (DCI) kuchunguza uhalifu huo.
Maafisa waliokamatwa wakiwemo James Lamata, Brian Kiplangat, Dad Sid, na Peter Kirui, walikuwa wakihudumu katika kituo cha KWS cha Samburu.
Waathiriwa walikuwa wametoka eneo la Lodogojek kabla ya kuvamiwa na maafisa hao ambao walikuwa katika gari la aina ya Land Cruiser.
Maafisa hao walikuwa wameibia KSh 9,500 miongoni mwa mali nyinginezo, kwa mujibu wa ripoti ya DCI.
Washukiwa hao walinaswa baada ya makachero wa DCI kuandaa kwenye gwaride.
Washukiwa watafunguliwa mashtaka ya wizi wa kimabavu.