This archive report was first published on 22 December 2019.
Mezi ya Disemba 21, 2019, mechi ya Kombe la Shirikisho kati ya vilabu vya Tanzania Young Africans (Yanga) na Iringa United ilisimamishwa baada ya kundi la nyuki kuvamia uwanja huo na kuwachochea wachezaji kuzua taharuki.
Wachezaji kutoka upande zote mbili walilala chini huku wengine wakichana mbuga.
Ali Mtoni Sonso, mchezaji mmoja wa Yanga, alijeruhiwa wakati wa tukio hilo na alitafuta huduma ya kwanza kutoka kwa benchi ya klabu kabla ya kurejea uwanjani.
Wakati huo huo, nyuki hao hawakuwazuia vijana wa Mwinyi Zahera kutwaa ushindi katika mechi hiyo huku wakisajili 4-0 dhidi ya wapinzani wao.