Skip to main content

Vita dhidi ya Waititu vilipangwa na katibu kwenye serikali ya kitaifa ▷ Nyakundi Report

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

This archive report was first published on 22 December 2019.

Waititu: Mchakato wa Kutimuliwa ulipangwa na Katibu wa Serikali ya Kitaifa

Uchakato wa kutimuliwa wa Gavana Ferdinand Waititu wa Kiambu ulipangwa na wakuu wa serikali pamoja na wafanyibiashara tajika. Kulingana na gazeti la Nation, Disemba 22, katibu mmoja kutoka Mt Kenya anayehudumu katika serikali ya kitaifa alihusika pakubwa katika mchakato huu.

Uchakato huo ulianza na mkutano uliofanywa katika ofisi za maafisa wa serikali kuu, ambapo maafisa wakuu waliamua kuwa kaunti ya Rais haifai kuwa na jina mbaya. Kwa hivyo, iliamuliwa kwamba gavana atimuliwe.

Katibu huyo, anayeonekana kuwa na ushawishi mkubwa kwenye serikali ya Rais Kenyatta, alikabidhiwa jukumu la kuhakikisha MCAs wa Kiambu wanapitisha kura ya kutokuwa na imani na Waititu.

Uchakato huo ulikuwa na matokeo mabaya kwa Waititu, ambaye alishtakiwa kwa matumizi mabaya ya afisi kwenye utoaji wa tenda za KSh 588M. MCA wa wadi ya Biashara Elijaha Njoroge aliambia gazeti hilo alikuwa mmoja wa waliotumiwa kuhakikisha Waititu anafurushwa mamlakani.

"Sitapumzika mpaka Waititu aondoke kama gavana wa Kiambu," Njoroge alisema.

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →