This archive report was first published on 21 December 2019.
Kituo cha Voi kilizuka baada ya demu kufukuzwa njia kuzomewa hadharani na mamake aliyemtaka akome tabia yake mbaya.
Umbea mtaani unasema kuwa mama alisinyika na mazoea ya kipusa kubadilisha wanaume kama nguo kwa kuwa kila kuchao aliwaleta wanaume tofauti nyumbani.
Alipomfumania mwanadada mjini akipiga gumzo na kalameni, mama aliwaka na kusema, "Kuanzia leo nisikuone tena na mwanamume. kama ni ymchumba mlete nyumbani umpendaye, sio kila mwanamume ni wako,".
Alipomkaripia vikali bintiye mbele ya jamaa, mama alisema kwamba amechoka kuona sura za wanaume tofauti wakiwa na binti yake hadi anachanganyikiwa ni nani haswa anachumbiana naye.
Alipomwuliza mamake amaye alikuwa amemkazia macho kupindukia, mama alinguruma na kumwacha kidosho na mshikaji wake na kusema, "Kama ni umalaya peleke danguroni iwapo hutaki kuwa na mchumba mmoja,".