This archive report was first published on 17 December 2019.
Kituo cha Cheptais, Bungoma, kilikuwa na tukio la kusisimua baada ya kakake kudai alikuwa mwizi sugu. Hii ilikuwa baada ya ndugu yake kufaulu mahojiano ya kuwa karani katika kiwanda kimoja eneo hilo.
Alipokuwa amefaulu mahojiano, jamaa alipewa kazi, lakini ilikuwa vigumu kwake kuanza kazi kwani nduguye wa toka nitoke alianza kueneza fununu kwamba kalameni alikuwa na tabia ya kuiba.
Alipojaribu kufuatilia ili ajue kilichotokea, aliarifiwa ni kakake ambaye anahudumu katika kampuni hiyo alimchongea baada ya kumuonya meneja dhidi ya kumuajiri.
"Msikubali aanze kazi. Ana tabia ya kuiba vitu kila mahali anapopewa kazi," nduguye jamaa alimwarifu meneja.