This archive report was first published on 13 December 2019.
Kitumbua kiliingia mchanga mganga alipoanza kumtishia jamaa kwa kukataa mahanjamu yake.
Alipandwa na mori na kukataa katakata kuingia boksi ya mama kwani kulingana naye walikubaliana amsaidie kisha aende zake.
Alipoweka kalameni alikataa kujibu na kumkataa kwa kusema, "Kubali yaishe! Kwa ndoga zangu naweza kukufanya usipate mke wa kuoa. Ukinikataa utaishia maisha ya kuhangaika. Yote tisa, kumi naitwa siendi popote upende usipende," alisema mganga.
Si hayo tu kwani mama alizidi kumrushia jamaa mistari ndiposa akumkubali kwani kulingana naye alikuwa angali mrembo na mwenye uwezo wa kumzalia watoto.
Penyenye zinasema kalameni aliondoka kwa hasira kwenda kuwasaka maboraboaro wenzake waje wamsaidie kumnyanyua mganga huyo kutoka chumbani mwake.
Alipoondoka, kalameni alisema, "Kwa nini unataka nirudi kwangu usiku huu. Kwani unanifukuza? Kumbuka kwamba mimi ni mwanamke kama wale wengine. Kwa taarifa yako siondoki ng'o," alisema.
Alipoweka kalameni alikataa kujibu na kumkataa kwa kusema, "Ondoka uende kabisa. Kama ulikuja kwangu kunitia majaribuni haiwezekani hata kidogo. Ulikuja hapa kunihudumia na wala sio mpango mwingine wa kukuoa," alinguruma.