This archive report was first published on 9 December 2019.
Video ya jinsi John Mutinda alivyotumbukia majini yaibuka baada ya kamera za CCTV kutoa ushahidi wa kina kuhusu kisa hicho.
John Mutinda alitumbukia majini Jumamosi, Disemba 7, saa 4:20 asubuhi, wakati alikuwa akiendesha gari lake kwa kasi.
Alipiga gari moto na kutoka kwa kasi baada ya kusema alikuwa amekutana na marehemu babake kwa ndoto na akamtaka wakutane katikati mwa mji wa Mombasa.
Mjane wake, Ruth Mueni, alisema alijaribu kumkataza Mutinda asifanye kama ndoto hiyo ilivyokuwa imemwagiza, lakini akakataa.
Video ya kisa hicho imeibuka baada ya kanda ya video inayoonyesha yaliyojiri katika kisa hicho kutoa ushahidi wa kina.