This archive report was first published on 4 December 2019.
Kituo cha habari cha Taifa Leo linaeleza kwamba kulizuka kwa pombe kati ya familia kutoka upande wa binti na jamaa baada ya kuanza kulumbana kuhusu mahari.
Uhasama ulizuka muda mfupi baada ya pombe waliyokuwa wakibugia kukolea.
Stimu zilipowapanda zaidi walinyosheana vidole na kuinuliana bakora wakitaka kutandikana kila mmoja wao akitaka kuonesha ubabe wake.
Penyenye zinasema vita vikali vilizuka mahali hapo na kuwalazimu majirani kuingilia kati na kudhibiti hali huku pombe ikitapakaa kila mahali.