Skip to main content

Walimu Wagoma Kwa Muda Kusahihisha Mtihani wa KCSE

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

This archive report was first published on 3 December 2019.

Walimu wengi wa Kenya waligoma kushiriki katika mchakato wa kusahihisha Mtihani wa KCSE, kwa kuwa walikuwa wakilalamikia mazingira duni ya utenda kazi.

Walimu hao walikuwa wakishiriki katika shule ya Machakos, ambapo walimu walikuwa wakilalamikia malipo ya KSh46 kwa kila karatasi, huku walikuwa wakihitaji KSh68.

Walimu hao pia walikuwa wakilalamikia mazingira duni ya utenda kazi, huku zaidi ya 700 kati yao walilazimika kulala sakafuni.

Polisi walitumwa katika vituo vya mtihani kukabiliana na walimu waliokuwa wakigoma.

Baraza la Kitaifa la Mitihani (Knec) lilifanya mkutano na walimu hao na kukubaliana kulipwa zaidi ya KSh52 kwa kila karatasi, lakini walimu hao wanaonekana kutoridhika.

Knec pia ilibadilisha mpango wake wa awali wa kuwatimua walimu 700 endapo hawakuridhishwa na malipo hayo, lakini badala yake kukubali kufanya mazungumzo nao.

Afisa Mkuu Mtendaji wa Knec, Mercy Karogo, alisema kwa sasa suala hilo limetatuliwa.

“Tumezungumza na kutatua suala hilo ambalo lilikuwa lemelemaza zoezi hili tangu siku ya Jumatatu,” alisema Karogo licha ya kuzomewa na walimu wenye hamaki.

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →