Skip to main content

Mwanahabari Erick Oloo alifariki baada ya kupigwa kwa kifaa butu kichwani

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

This archive report was first published on 23 November 2019.

Mwanahabari Erick Oloo alifariki baada ya kupigwa kwa kifaa butu kichwani

Imebainika kuwa Erick Oloo, mwandishi wa The Star, alifariki baada ya kupigwa kwa kifaa butu kichwani na tumboni, kufuatia upasuaji wa maiti wake mnamo Jumamosi, Novemba 23, 2019.

Upasuaji wa maiti ulifichua kwamba marehemu alifariki baada ya kuvuja damu nyingi alipopigwa na kifaa butu kichwani na tumboni.

Imebainika kuwa Erick Oloo alikuwa na uhusiano wa mapenzi na Sabina Kerubo, naibu OCS wa kituo cha Ugunja, ambaye inadaiwa ni mpenziwe.

Imebainika kuwa Erick Oloo alikuwa na makabiliano na wanaume wengine katika chumba cha Kerubo kabla ya kifo chake kutokea.

Naibu OCS Kerubo, bintiye, mfanyikazi wake na jamaa aliyetambulika kama Victor walikamatwa kuhusiana na mauaji hayo.

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →