Skip to main content

Kizaazaa Bungeni: Didmus Baraza Kutishia Kumnyorosha Gladys Wanga

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

This archive report was first published on 22 November 2019.

Kizaazaa Bungeni: Didmus Baraza Kutishia Kumnyorosha Gladys Wanga

Alhamisi, Novemba 21, 2019, kizaazaa kilishuhudiwa bungeni baada ya wabunge Didmus Baraza wa Kimilili, Gladys Wanga wa Homa Bay, na Esther Passaris wa Nairobi kutupiana cheche za maneno.

Utata ulianza wakati wa mjadala wa ripoti ya kamati ya bunge kuhusu kanda ya video ya ufuska iliyohusu mbunge Fatuma Gedi.

Didmus Baraza alizua kizaazaa bungeni baada ya kutishia kuwa kopi wenzake. Picha: Standard

Kamati hiyo ilitoa ripoti yake na kutaka Gedi achukuliwe hatua na bunge kwa kosa la kufichua hatua ya wachunguzi wa DCI kwa wabunge wenzake.

Baraza alitishia kuwapa kofi wabunge Gladys Wanga na Esther Passaris baada ya kutishia kumnyorosha Wanga.

Baraza alisema, "Bwana Spika nilinde kutokana na Gladys Wanga ambaye anapiga kelele. Bwana Spika, nitamnyorosha huyu dada kwa sababu ananipigia kelele," Baraza alisema.

Passaris naye alikerwa na kuamka huku akimtupia maneno makali mbunge huyo kwa kutishia kumpa kofi Wanga.

Didmus Baraza alitishia kumpa kofi Esther Passaris.

Spika Justin Muturi alituliza hali na mjadala ukaendelea bila sokomoko za watatu hao.

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →