This archive report was first published on 17 November 2019.
Naibu Rais William Ruto alikuwa kwenye mtandao wa Twitter Jumapili, Novemba 17, 2019, akisema kuwa kuna njama kati ya wanahabari na mahasimu wa Jubilee katika kuvunja chama hicho.
DP Ruto alisema baada ya Rais Uhuru Kenyatta kukariri kuwa chama cha Jubilee kiko imara, mahasimu wao sasa wameanza kuweka mikakati mingine wakitumia wanahabari.
Alisema njama iliyopo ni kuhakikisha kuwa wanahujumu chama cha Jubilee.
Wanamtandao walimjibu DP Ruto wakisema kuwa amekuwa akionyesha hasira sana kupitia mtandao wake.
Mbunge wa Ainabkoi William Chepkut alimwambia DP kuwa sasa anageuka na kuwa Trump wa Kenya.
David Ndii, mwanaharakati, alizua hisia kali baada ya kutania Rais Uhuru Kenyatta.
Ndii alisema Rais Kenyatta yungali anaishi kwenye nyumba ya familia na kwa hivyo hafai kuongea wakati ambapo vijana wengine walijikakamua na kupata mali yao.