This archive report was first published on 15 November 2019.
Wafuasi wa Sarah Hassan na DJ Pierra Makena wamesubiri kwa hamu kuwaona warembo hao kwa pamoja tena wakiwatumbuiza. Warembo hao wamekuwa wakipendwa sana na wafuasi wao kwa sababu ya kazi zao za kipindi cha Tahidi High.
Warembo hao walitangaza habari hiyo njema kupitia mtandao wa Instagram ila hawakupatiana maelezo zaidi kuhusu filamu hiyo.
"Nimefurahia sana kurudi kwenye televisheni, filamu mpya yaja, Sarah, hatujaigiza pamoja kwa muda mrefu tangu siku zile tulipoigiza katika kipindi cha Changes', Pierra aliandika Instagram.
"Hatimaye tumekutana tena, nilikuwa nimekukosa sana rafiki wangu," Sarah alimjibu Pierra.
Wafuasi wao sasa wamesubiri kwa hamu kuwaona warembo hao kwa pamoja tena wakiwatumbuiza.