This archive report was first published on 15 November 2019.
Rais Uhuru Kenyatta amemlazimu Naibu Wake William Ruto kupangua ziara yake ya eneo la Mlima Kenya baada ya kuandaa mkutano na wabunge wa Mt Kenya.
Hiyo ni baada ya Ruto ahudhurie hafla ya harambee kaunti ya Nyeri lakini ikapanguka kutokana na mkutano wa Rais.
Ikulu ilimlaa ghafla viongozi wote wa Mlima Kenya kwenye mkutano wa faraghani ili kujadili masuala tata.
Wengi wanashuku kuwa siasa za 2022, mgawanyiko ndani ya Jubilee, suala la BBI na handisheki ndio zitazungumziwa na mdosi wa sasa wa Mt Kenya.
Hiyo ni baada ya Ruto alilazimika kupangua ziara yake katika kaunti za Kirinyaga na Murang'a alipokuwa anatarajiwa kuhudhuria hafla za kanisa baada ya kubainika kuwa Rais alikuwa ahudhurie ibada katika kanisa la ACK Kenol.
DP Ruto alikuwa amealikwa katika mchango wa kanisa na mbunge wa Kandara Alice Wahome na hivyo kulazimika kukosa kwenda na badala yake kumtuma mwakilishi.