Skip to main content

Mwenzetu Njenga Mswahili alikuwa na msongo wa mawazo, alitaka msaada lakini hakuna aliyemsaidia - Eric Omondi

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

This archive report was first published on 12 November 2019.

Mwenzetu Njenga Mswahili alikuwa na msongo wa mawazo, alitaka msaada lakini hakuna aliyemsaidia - Eric Omondi

Eric Omondi amesikitika na kusema jinsi mchekeshaji wa Churchill show, Anthony Njenga Mswahili alivyokuwa akisumbuka.

Alipatikana ameaga dunia Alhamisi, Novemba 7, eneo la Soko la Ndonyo mtaani Dagoretti South, na anadaiwa kugongwa na treni.

Eric Omondi anasema Njenga Mswahili alikuwa na msongo wa mawazo na alitafuta msaada lakini hamna aliyemsaidia.

Alisema wengi walifahamu kuhusu hali ya Mswahili na kifo chake kimemuumiza kwa kuwa alishuhudia kikimfika kuanzia miaka mitatu.

"Njenga alikuwa anatuilia lakini sote - nikiwamo, hatukumsaidia, ni kama hatuna utu tena," alisema Omondi.

Ingawa kifo cha Mswahili hakijafahamika vyema kilitokea vipi, kuna madai kuwa huenda alijiua kutokana na matatizo aliyokuwa akiyapitia.

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →