Skip to main content

Matiang'i, Mutyambai wachukua hatua kufuatia udhalimu wa polisi dhidi ya wanafunzi wa JKUAT

N

Nyakundi Report

Newsroom 2 min read

This archive report was first published on 12 November 2019.

Matiang'i, Mutyambai wachukua hatua kufuatia udhalimu wa polisi dhidi ya wanafunzi wa JKUAT

Chuo Kikuu cha JKUAT kimefungwa kwa sasa kufuatia ghasia za wanafunzi, na Inspekta Mkuu wa Polisi Hillary Mutyambai ameamrisha uchunguzi kuanza mara moja kuhusiana na udhalimu wa maafisa wa polisi dhidi ya mwanafunzi wa chuo hicho.

Video inayosambaa mitandaoni inaonyesha polisi wakitumia nguvu kupita kiasi dhidi ya wanafunzi wa JKUAT, na Mutyambai amesema atatumia saa 24 kuwakamata polisi waliohusika na hii ni baada ya umma kulalamika.

Polisi waliitikia wito baada ya ghasia zilizokuwa zikiendelea JKUAT, na Inspekta Mkuu amesema hii ni sehemu ya kazi yao la kuhakikisha sheria na amani vinazingatiwa.

Alisema, polisi wamepewa mafunzo kuhusu kuheshimu haki za binadamu na kila mara wapo chini ya amri kuzuia uhalifu kwa kutumia nguvu kulingana na hali ya wakati huo.

Alisema, "Ni bora kufahamu kuwa maafisa wote wa polisi wamepitia mafunzo ya hali ya juu ya kazi kuhusu jinsi ya kukabiliana na ghasia na mikutano isiyotakiwa."

Alisema, "Pia wamepewa mafunzo kuhusu kuheshimu haki za binadamu na haki za uhuru, na kwamba, kutumia nguvu ni lazima iwe kwa sheria na utashi wa haki; ni lazima kutumika kwa viwango vinavyostahili kwa kuzingatia uzito wa kosa na kwa kuwajibikia."

Awali, Waziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiang'i alikuwa ametoa tamko na kusema ofisi yake inashughulika baada ya umma kulalamika kuhusu nguvu zilizotumiwa na polisi kwa wanafunzi.

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →