This archive report was first published on 6 November 2019.
Wakazi wa Kiambu wamekabiliwa na kesi ya ufisadi inayohusu Gavana Ferdinand Waititu, mke wake Susan Wangari, na watu wengine wanane kuhusiana na ubadhirifu na kupotea kwa KSh 580.
Utata unaomzunguka Gavana Waititu unajirudia baada ya kundi la wanaharakati linalojiita "Okoa Kiambu" kuwasilisha barua katika bunge la kaunti hiyo ili kufanikisha mchakato wa kumng'atua.
Wanaharakati hao wamekusanya saini 200,000 katika kutafuta kumng'atua Baba Yao ambazo wamewasilisha katika bunge la kaunti.
Kesi dhidi ya gavana huyo sasa inatazamiwa kuanza Januari 21 hadi Februari 6, 2020.