This archive report was first published on 4 November 2019.
Uchunguzi wa kina unapendekeza kwamba kuna mambo ya ajabu sana ambayo hutokea jua linapochomoza na hata usiku unapoingia.
Matukio ya kushangaza na mengine yanayotufanya kugundua yaliyokuwa yamejificha hutokea kila wakati.
Uganda, nchini Magharibi, kuna jamaa ambaye amewaacha familia na jamaa zake katika mshangao mkubwa baada ya kutoa agizo la ajabu kuhusu matanga yake.
Aliwaagiza wapendwa wake kuwa, wakati wa kumuomboleza, wacheze na kuimba wimbo wa muimbaji mmoja tu ambaye ni John Kasandha, anayejulikana kama John Blaq.
Aliwataka vibao vyake vya 'African Boy' kupigwa katika matanga yake akifa, na ilifanyika hivyo.
Wakati wa kutimizwa kwa mapenzi hayo, John Blaq alichukua nafasi na kuipakia video ya shughuli ya matangani.
Chini yake aliandika: "Lala salama Jajja Augustine Mukoma. Mapenzi yako yalikuwa ni wimbo huu kupigwa katika matangani yako".
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsApp: 0732482690.