This archive report was first published on 1 November 2019.
Waihiga Mwaura atakuwa mtangazaji wa News Night kuanzia Jumanne, Novemba 5, baada ya Hussein Mohammed kujiuzulu kwa Royal Media Services.
Waihiga Mwaura ni mwandishi wa habari na mtangazaji wa Citizen TV katika kipindi cha habari cha Monday Report, akishirikiana na Trevor Ombija na Mashirima Kapombe.
Alijishindia tuzo ya BBC ya Komla Dumor mnamo 2018, na kuwa mwanamume wa kwanza kujinyakulia tuzo hiyo.
Waihiga Mwaura atachukua nafasi ya Hussein Mohammed, ambaye alijiuzulu baada ya kuhudumu kwa miaka 10 na kujitangaza kwa kipindi cha News Night.
Aliwaeleza mashabiki zake Ijumaa, Oktoba 4, kwamba alijiuzulu kutoka shirika la Royal Media Services ili kushughulikia mambo fulani ya kibinafsi.