Skip to main content

Familia ya Mzee Moi Yatangaza Madai Yanaenezwa Kuhusu Afya Yake Ni Uongo

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

This archive report was first published on 31 October 2019.

Madai yanaenezwa kuhusu afya ya rais mstaafu Daniel Moi kwa sasa yamekataliwa na familia yake.

Amesema hili Msemaji wa familia Mzee Moi, Bw. Lee Njiru, katika taarifa yake ya juma hii.

Alisema kwamba uvumi unaosambaa kuhusu afya ya Mzee Moi ni uongo na kwamba rais mstaafu bado anapokea matibabu katika Nairobi Hospital.

“Taarifa zozote kuhusu rais mstaafu mzipuuze hadi tutakapotia taarifa rasmi itakayofuata njia inayofaa,” Njiru alisema.

Alisema pia kwamba kuna njia zifaazo zitakazotumika taarifa za aina hiyo na hivyo ni lazima kukoma kueneza uvumi na uongo kuhusu hali ya afya ya Mzee Moi.

Aliongeza kwamba yeye ndiye Katibu wa Habari za mstaafu Daniel arap Moi na yeye ndiye msemaji wa familia hiyo.

“Mimi ndiye Katibu wa Habari za mstaafu Daniel arap Moi na mimi ndiye msemaji. Usiposikia kutoka kwangu jua mengine yote utakayosikia ni uongo,” Njiru aliongeza.

Alisema kwamba Mzee Moi alilazwa Nairobi Hospital Jumamosi, Oktoba 26, baada ya kuwa na matatizo ya kupumua.

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →