Skip to main content

FKF Rais Nick Mwendwa Amegeuzia Mishale Katibu wa Michezo Kirimi Kaberia

N

Nyakundi Report

Newsroom 2 min read

This archive report was first published on 29 October 2019.

FKF Rais Nick Mwendwa Amegeuzia Mishale Katibu wa Michezo Kirimi Kaberia

FKF Rais Nick Mwendwa amemlipua Katibu wa Michezo Kirimi Kaberia kwa kusema amekataa kuzipa timu za kitaifa pesa za kushiriki mashindano ya kimataifa.

Alisema hili Jumanne, Oktoba 29, 2019, wakati akizungumza na wanahabari jijini Nairobi.

Alidai kuwa Kaberia, ambaye ndiye msimamizi wa fedha katika Wizara, mara kwa mara amekataa kujibu wakati akitakiwa kuipa pesa timu ya wanawake ya Harambee Starlets.

Alisema pia kuwa Kaberia alikataa kuachilia pesa kwa ajili ya timu ya soka ya wanaume, Harambee Stars, tangu iliposhiriki mashindano ya 2019 ya Kombe la Bara Afrika nchini Misri mnamo Julai mwaka huu.

Alisema, "Rais alisema sasa kuna mfuko wa pesa za michezo ambazo zitatumika kwa ajili ya timu za kitaifa. Lakini katibu amekataa kuzifadhili timu hizi. Sijui ana shida gani na soka," Mwendwa alisema.

Alisema pia kuwa, "Haudhurii mechi za Harambee Stars kwa sababu kila mara amewaahidi pesa, lakini ahadi zake hazitimii," alisema.

Alisema kuwa hii ni sababu ya kufutilia mbali kambi ya mazoezi kwa timu ya Starlets ambayo ilikuwa ikijiandaa kwa mchuwano wa kufuzu Olimpiki 2020 wiki ijayo dhidi ya Zambia mechi iliyotarajiwa Nairobi kisha Lusaka.

Alisema pia kuwa, hali ikiwa ni hiyo basi Harambee Stars haitashiriki michuwano ya kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika 2021 dhidi ya Togo na Misri jijini Nairobi na Cairo.

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →