Skip to main content

Afisa wa Utawala aliyekamatwa kwa kuhifadhi sare za polisi kuzuiliwa kwa siku nne zaidi

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

This archive report was first published on 29 October 2019.

Afisa wa Utawala aliyekamatwa Ijumaa, Oktoba 25 kwa kuhifadhi sare za polisi katika chumba chake eneo la Mihango mtaa wa Kayole amezuiliwa kwa siku nne zaidi.

Afisa huyo aliyetambulika kama David Odhiambo atazuiliwa katika kituo cha polisi cha Kayole huku uchunguzi zaidi ukiendelea.

Alisimamishwa kazi kwa muda baada ya kupatikana na hatia ya uhalifu na mahakama ya Malindi.

Uchunguzi ulianza baada ya makachero kutoka Idara ya Upelelezi kuyafumania makazi yake na kumnasa na bidhaa hizo.

Alinasa bidhaa kama sare za polisi wa Utawala, pingu, kofia, viatu, bendera za polisi na mali nyinginezo.

Uchunguzi uliendelea baada ya afisi ya DCI kuiomba mahakama kumzuilia mshukiwa kwa siku tano.

Alipokubaliwa kwa ombi hilo, mshukiwa atazuiliwa kwa siku nne huku uchunguzi zaidi ukiendelea.

Atatarajiwa kufikishwa mahakamani Novemba 1.

Maafisa wa polisi wanaohudumu katika kituo cha Kayole walidaiwa kuhusika na uhalifu ambao ulipelekea mfanyibiashara mmoja kupoteza KSh 6 milioni katika chumba cha kukodisha cha kulala.

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →