Skip to main content

Rais Uhuru na Ruto Wataka Watahiniwa wa KCPE Kila La Heri

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

This archive report was first published on 29 October 2019.

Rais Uhuru na Ruto Wataka Watahiniwa wa KCPE Kila La Heri

Rais Uhuru Kenyatta na naibu wake William Ruto wameongoza taifa kwa kuwatakia watahiniwa wa darasa la nane katika Mtihani wa Kitaifa wa Shule za Msingi (KCPE) uliofungua Jumanne, Oktoba 29, 2019.

Watahiniwa hao wamekuwa wakijitahidi kufanya vizuri katika mtihani huo, na rais Uhuru na Ruto wamehimiza kujiepusha na udanganyifu wa mtihani na kutumia kile walichofunzwa darasani.

"Maombi yangu ni kuwatakia kila la heri watahiniwa wote watakaofanya mtihani wa KCPE na KCSE. Kama nilivyowambia, mtihani sio mwisho wa maisha lakini hatua katika ndoto zenyu. Walimu wote, wazazi na Wakenya kwa jumla wako pamoja nanyi katoka kipindi hiki," alisema rais Uhuru.

Rais Uhuru pia aliongeza kuwa serikali yake imejitolea kuhakikisha kuwa watahiniwa wote wanapata nafasi kuendeleza masomo yao katika Shule ya Upili, chuo kikuu, chuo cha elimu na pia shule ya kiufundi (TVET).

"Ninawaamni na pia najua mumepewa elimu ya kutosha na habari kuhusu kibarua kinachowasubiri. Juhudi zote na pia kujitolea ili kuhakikisha kuwa munafaulu," aliongeza rais Uhuru.

Naibu wa rais William Ruto aliwatakia watahiniwa heri njema katika mtihani huo wa kitaifa akiwa na imani kuwa watafaulu.

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →