This archive report was first published on 25 October 2019.
Alhamisi, Oktoba 24, mwili wa mtoto wa miaka 13 wa mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Nairobi Hannah Khahugani ulipatikana nyumbani kwake, na upasuaji ulifanyika katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Chiromo.
Upasuaji huo ulionyesha kuwa mtoto huyo alikuwa na vidonda tumboni ambavyo vilisababisha damu kuvuja.
Khahugani alitiwa nguvuni kwa kuiweka maiti ya mtoto huyo ndani ya nyumba yake kwa siku kadhaa, na baada ya polisi kufahamishwa kuhusu tukio hilo, walifika na kumkamata mhadhiri huyo wa Chuo Kikuu anayefundisha somo la unesi.
Stephen Mwangi, mtunzaji wa ghorofa ambaye anapoishi nyumbani kwa mhadhiri huyo, alisema kuwa alikuwa nimefuata kodi ya nyumba na ndiposa nikachungulia dirishani na kukutana na nzi na harufu kali.
Khahugani alidai kuwa mtu wa imani kali na aliyekuwa ameingia ndani ya dini yake, na mmoja wa majirani alisema kuwa alikujitenga na familia na marafiki, na kuzungumzia kuhusu mwisho wa dunia.