This archive report was first published on 25 October 2019.
Alhamisi, Oktoba 24, mvua kubwa ilianza kunyesha eneo la Tsavo, kusababisha mafuriko makubwa na kufanya mabasi mawili ya shule yaliokuwa yamewabeba wanafunzi yakwama katika mbuga ya wanyama ya Tsavo.
Shule hizo hazijatambulika, lakini mashirika ya msalaba mwekundu na KWS yanawajibika kudhibiti hali.
Idara ya hali ya anga ilitoa tahadhari kuhusu kushuhudiwa kwa mvua kubwa katika maeneo mbali mbali ya nchi, ambayo itaendelea hadi Jumapili Oktoba 28.
Tayari watu 29 wameripotiwa kufariki dunia huku zaidi ya 11,000 wakipoteza makazi kutokana na mafuriko.