This archive report was first published on 24 October 2019.
Wakenya wamlima DP Ruto kwa kuzindua stima kwenye nyumba za matope ¶
Naibu Rais William Ruto alizindua stima kwenye nyumba za matope huko kaunti ya Narok, kati ya wakazi wa Sekenani, ambao wanaishi maisha ya uchochole sana.
Wakazi hao walishangaa kama wanahitaji umeme kama vile wanahitaji makazi bora, na baadhi yao walihisi kuwa serikali ingehakikisha kuwa wakazi kwanza wana makao mazuri kabla ya kuwaunganisha na umeme.
Walihisi kuwa umeme huo utakuwa ni hatari kwa wakazi kutokana na hali ya nyumba zao na kwa hivyo serikali ina jukumu la kuhakikisha wakazi hao wanapata nyumba nzuri.
Walihisi kuwa ilikuwa sawa kwa serikali kufikisha umeme katika kila kona ya Kenya pasi kubagua yeyote.
Naibu Rais William Ruto alipata ukaribisho kwa kikombe cha maziwa ya kidesturi ya jamii ya wamaasai kabla ya kuenda katika hafla zingine.
Wakenya hao walihisi kuwa serikali ingehakikisha kuwa wakazi kwanza wana makao mazuri kabla ya kuwaunganisha na umeme.
Walihisi kuwa umeme huo utakuwa ni hatari kwa wakazi kutokana na hali ya nyumba zao na kwa hivyo serikali ina jukumu la kuhakikisha wakazi hao wanapata nyumba nzuri.
Walihisi kuwa ilikuwa sawa kwa serikali kufikisha umeme katika kila kona ya Kenya pasi kubagua yeyote.