This archive report was first published on 21 October 2019.
Sherehe za Mashujaa zilishuhudia kushindana kati ya Naibu Spika wa Kaunti ya Trans Nzoia David Kaboloman na Mbunge wa Saboti Caleb Amisi wakati wa sherehe za Mashujaa katika kaunti hiyo.
Naibu Spika Kaboloman alikashifu Mbunge Amisi kwa kutokuwa na rekodi yoyote ya maendeleo katika eneo lake, huku akitaja barabara mbovu zisizopitaka katika eneo bunge lake.
Amisi alijibu kwa kumuelezea kama mpiga kelele na kumkashifu kwa kueneza siasa, na hii ilimfanya Kaboloman kumkaribia na kumshika kwa shingo kabla ya Kamanda wa Kaunti hiyo Ali Ayub na maafisa wengine wa polisi kuwatawanya.
Polisi walimsukuma spika huyo mwenye hamaki huku Kamishna wa Kaunti Sam Ojwang akijaribu kuleta utaratibu.
Sam Ojwang alikashifu kitendo hicho kwa kukitaja kama siha kwa viongozi kupigana hadharani.
Sherehe za Mashujaa zilishuhudia kushindana kati ya Naibu Spika wa Kaunti ya Trans Nzoia David Kaboloman na Mbunge wa Saboti Caleb Amisi wakati wa sherehe za Mashujaa katika kaunti hiyo.