This archive report was first published on 18 October 2019.
Alhamisi, siku ya watu kunywa pombe na kujiburudisha ili kusherehekea rekodi ya Eliud Kipchoge, mteja mmoja alikataa kulipa bili ya KSh 600 kwa pombe aliyokunywa kwa sababu ilikuwa ya bwerere.
Alipokataa kulipa, mvutano ulizuka baina yake na mwenye baa aliyetishia kumpa kichapo kikali asipotoa pesa hizo.
"Lipa bili buda. Pombe ya bure hakuna hapa!" alikuwa na maoni ya mwenye baa.
Alipokataa kulipa, mteja huyo alipiga simu marafiki zake ambao walimtumia Mpesa akalipa bili hiyo kabla ya kuondoka.
Maandamano hayo hayo yalifanyika mji wa Eldoret, ambapo watu wengi walikuwa wakimpongeza Eliud Kipchoge kwa kufikia rekodi kubwa ya kilomita 42 chini ya saa mbili mjini Vienna, Austria.