This archive report was first published on 17 October 2019.
Paul Pogba na De Gea wabanduliwa katika mechi dhidi ya Liverpool ¶
Paul Pogba na David De Gea wamebanduliwa kwa ajili ya mechi ya Ligi Kuu dhidi ya Liverpool baada ya kujeruhiwa katika mechi za zamani.
De Gea alifanyiwa uchunguzi wa kimatibabu siku ya Jumanne, Oktoba 15, baada ya kukumbana na jeraha katika mechi ya kufuzu kwa michuano ya Euro 2020 kati ya Uhispania na Uswidi.
De Gea hatakauwa fiti kwa mechi hiyo ya wikendi, na Pogba pia hajapata nafuu tangu kufanyiwa skana baada ya mechi dhidi ya Arsenal.
"David anahitaji kufanyiwa skana. Nafikiri hatakuwepo. Hata hivyo, ilikuwa thibitisho jana usiku. Paul alifanyiwa skana baada ya mechi dhidi ya Arsenal. Huenda akakosa kukawia sana, lakini hii mechi hapana," alisema kocha Ole Gunnar Solskjaer.
Paul Pogba hajashiriki mechi tano ya Man United kwa sababu ya msururu wa majeraha msimu huu.
Wachezaji 10 wa Mashetani Wekundu wako mkekani kwa kuuguza majeraha huku Anthony Martial, Aaron Wan-Bissaka na Jesse Lingard wakiwa miongoni mwao.
De Gea na Pogba watakuwa bila huduma katika mechi ya Ligi Kuu dhidi ya Liverpool.