This archive report was first published on 15 October 2019.
Alhamisi, Oktoba 14, 2019, mmiliki wa shule ya msingi ya Precious Talent Academy Moses Wainaina Ndirangu alishtakiwa kwa kosa la kuwaua wanafunzi wanane bila kukusudia.
Wainaina alikamatwa baada ya kukana mashtaka hayo, na akachukuliwa kwa dhamana ya KSh 500,000 na mdhamini kiasi sawia na hicho.
Alishtakiwa kwa kutekeleza mauaji bila kukusudia, na alikamatwa kufuatia shinikizo la viongozi kadhaa wakiwemo seneta wa Laikipia John Kinyua na Spika wa seneti Kithure Kindiki.
Waziri wa Elimu Magoha alifutilia mbali leseni ya shule hiyo na hata kuifunga huku akiagiza wanafunzi wake 800 kuhamishwa hadi shule za umma zilizokuwa karibu na eneo hilo.
Shughuli ya uokoaji baada ya majengo ya Shule ya Precious Talent kuporomoka.
Wainaina alisema mkasa uliowaua wanafunzi ulifanyika kutokana na mapenzi ya mwenyezi Mungu, na alikamatwa kufuatia shinikizo la viongozi kadhaa wakiwemo seneta wa Laikipia John Kinyua na Spika wa seneti Kithure Kindiki.