Skip to main content

Tob Cohen Mwili Uliopatikana Uonesha Alifariki Baada ya Kupigwa na Kifaa Butu Kichwani

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

This archive report was first published on 4 October 2019.

Upasuaji wa maiti wa Tob Cohen, mfanyabiashara wa Kiholanzi, umefichua kuwa alifariki baada ya kupigwa na kifaa butu mara kadhaa kwenye mwili wake.

Alipatikana maiti yake ndani ya tanki la ardhini Septemba 13, na upasuaji ulifanywa kwa mwili wake Jumatano, Septemba 18.

Uchunguzi wa maiti ulionesha kuwa Cohen alifariki baada ya kupigwa na kifaa butu kichwani, na kuwa na majeraha mabaya ya upande wa kulia wa kichwa chake, mbavuni na usoni.

Alhamisi, Oktoba 3, mkewe Sarah Wairimu alikana mashtaka dhidi ya mauaji ya mumewe mbele ya Jaji Stella Mutuku na wakati uo huo kuomba mahakama imwachilie kwa dhamana.

Wairimu, ambaye ni mshukiwa mkuu wa mauaji ya Tob Cohen, inasemekana alimuua Cohen kati ya Julai 19 na 20 akishirikiana na wenzake siku ambayo mfanyabiashara huyo aliripotiwa kupotea.

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →