Skip to main content

Mtangazaji Hussein Mohammed Ajiuzulu baada ya Miaka 10

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

This archive report was first published on 4 October 2019.

Mtangazaji wa Citizen TV, Hussein Mohammed, amejiuzulu kutoka kwenye kituo cha televisheni kilichomilikiwa na Royal Media Services baada ya miaka 10 ya huduma.

Kwa ujumbe aliouchapisha Facebook Ijumaa, Oktoba 4, 2019, Hussein alidokeza kuwa amejiuzulu kutoka kwa fani hiyo ili kushughulikia mambo fulani ya kibinafsi.

Aliwashukuru wafanyikazi wenzake kwa ushirikiano waliokuwa nao kazini na kuhakikisha kuwa atakuwa na muda wa kujipumzisha baada ya Oktoba.

"Miaka hii kumi imekuwa ya kufana kwangu nikihudumu Citizen TV. Tumejumuika na kufurahia na wafanyikazi wenzangu kazini RMS. Nimeamua kujiuzulu na kujipumzisha kwa muda ifikiapo Oktoba In Sha Allah ili nishughulikie masuala mengine. Niliwapenda mashabiki, wakosoaji na kila mara nilipokuwa kazini. Tutaonana tena karibuni," alisema.

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →