This archive report was first published on 3 October 2019.
Maafisa wa polisi watano wa Kitui waliokamatwa Jumatano, Oktoba 2, 2019, baada ya kupatikana wakisafirisha bangi pamoja na bidhaa zingine zinazoshukiwa kuwa haramu.
Waliokamatwa hao walitiwa mbaroni katika soko la Kanyonyoo kwenye barabara ya Garissa-Thika Highway.
Maafisa wa polisi walikamatwa na bangi kwenye barabara ya Garissa-Thika. Picha: Standard
Maafisa wa polisi walikuwa na mifuko 68 ya bangi iliyokuwa ikisafirishwa kwenye gari la polisi, pamoja na shilingi 239,500 na kilo 300 za mchele.