This archive report was first published on 2 October 2019.
Familia ya Mariam Kighenda na mwanawe Amanda Mutheu ililazimika kutafuta usaidizi wa kibinafsi baada ya kuzama baharini Mombasa.
Kwa mujibu wa John Wambua, mumewe wa Kighenda, familia ililazimika kutafuta usaidizi wa kibinafsi wa wana maji ambao wanaweza kusaidia kupatikana kwa miili ya familia yake.
Akiongea na wanahabari Jumanne, Oktoba 1, Wambua alisema kama familia wanazidi kuteseka kutokana na hali ya kutafuta miili hiyo kujikokota.
Aliteta kuwa serikali imeshindwa kuwasaidia tangu Jumapili, Septemba 27 wakati ambapo mkasa huo ulitokea.
Kufikia Jumatano, Oktoba 2, wawili hao hawakuwa wameptakina na familia ililazimika kutafuta usaidizi wa wapiga mbizi kutoka Afrika Kusini.
Familia ya mama na mwana waliozama baharini Mombasa. Picha: Citizen TV