Skip to main content

Mumewe Mariam asimulia mawasiliano yao ya mwisho na mkewe kabla ya mkasa wa Likoni

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

This archive report was first published on 1 October 2019.

John Wambua, mume wa Mariam Kighenda, alikuwa mtandaoni Twitter wakati alipoona taarifa kwamba kulikuwa na mkasa wa gari kuzama baharini Likoni.

Alipokuwa mtandaoni, alipiga simu kwa mkewe Mariam, lakini hakupatikana.

Wambua alisema kuwa, Mariam alinipigia simu na kuwaelezea kuwa walikuwa wakaribia kuvuka Likoni, lakini aliondoa kuwaferi baada ya kuona taarifa ya mkasa wa gari kuzama baharini.

Wambua alisema kuwa, Mariam alikuwa akirejea Mombasa kutoka kaunti ya Kwale ambapo alikuwa amezuru shamba lao kabla ya gari la mkasa kuzama baharini.

Ujumbe kutoka huduma za feri ulithibitisha kuwa gari lililokuwa limezama lilikuwa na uasjili wa KCB 289C, gari ambalo Wambua alisema lilimilikiwa na mkewe.

Walioshuhudia ajali hiyo walisema kuwa gari la Mariam lilitumbukia katikati ya Bahari, na Mariam na mwanawe Amanda walionekana wakipunga mikono hewani huku wakipiga mayowe kuomba usaidizi kabla ya gari hilo kuelea kwa takriban dakika 20 na kuzama.

Shughuli za kuwaokoa zilisitishwa baada ya giza kuingia, huku ikisemekana kuwa gari hilo limeonekana mita 60 ndani ya bahari.

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →