Skip to main content

Wabunge Wataka Kudhibiti WhatsApp na Facebook

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

This archive report was first published on 24 September 2019.

Wabunge wameudhika baada ya mbunge wa Malava Malulu Injendi kutengeneza mswada unaopanua kudhibiti mitandao ya WhatsApp na Facebook.

Msukumo wa mswada huo ni kuhakikisha kwamba wote wanaotaka kuanzisha vikundi kupitia WhatsApp na Facebook watalazimika kutafuta leseni kwanza kwa shirika la kudhibiti mawasiliano nchini (CAK).

Wabunge hawa wameongozwa na Babu Owino, ambaye alisema kuwa mswada huo ni upuzi na huwezi kuwanyima vijana uhuru wao wa kuongea kama walivyohakikishiwa kwenye katiba.

"Huo ni upuzi. Huwezi kuwanyima vijana uhuru wao wa kuongea kama walivyohakikishiwa kwenye katiba," Babu Owino alisema.

Wabunge wengine wameeleza kuwa Wakenya wanafaa kufanya mageuzi ya kikatiba na kubadilisha viti vya ubunge kwani baadhi ya wabunge hawajui wanalofaa kufanya.

Wakati wa kujadili mswada huo, wabunge wameuliza Malulu kutafuta mswada mwingine kwani bunge haliwezi kujadili mswada wa kiwango hicho.

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →