This archive report was first published on 18 September 2019.
September 18, 2019 - Mpelelezi binafsi Jane Mugo ameshtakiwa kwa makosa mawili ya kutishia kuwaua watu wawili tofauti.
Aliwasilishwa mahakamani Jumatano, Septemba 18 na alishtakiwa kwa kumtishia kumuua Patrick Mugasia Kefa na Deepa Shah.
Maafisa wa polisi walisema kuwa Mugo aliitwaa bastola yake na kumtishia kumpiga risasi Kefa mnamo Agosti 15, 2015, na kosa la pili lilifanyika katika eneo la Kyuna Close, Spring Valley Februari 4, 2019, ambapo alitishia kumuua Shah.
Aliachiliwa kwa dhamana ya KSh 300,000 baada ya kukana mashtaka na kufikia makubaliano na maafisa wa polisi.
Alitakiwa kufika katika afisi za DCI chini ya saa sita baada ya kuachiliwa na kuhakikisha kuwa amesalimishe bastola hizo na cheti cha kuzimiliki.
Ukosoaji wa kesi hii utasikizwa tena Octoba 15 na Octoba 16 mtawalia.