This archive report was first published on 18 September 2019.
Jimmy Gait, mwanamuziki tajika wa nyimbo za Injili, amefichua habari za kusikitisha kuwa atastaafu muziki hivi karibuni.
Alirekodi wimbo wake wa mwisho wakati alipokuwa akipokea matibabu nchini India.
Wimbo huo utakuwa wa mwisho katika taaluma yake ya muziki kwani atakuwa akiondoka nyanja hiyo ya muziki.
Alisema alitumia muda wake kurekodi wimbo huo na kwamba itatangazwa baada ya kuzindua video ya wimbo huo.
Jimmy Gait alikuwa nchini India kwa matibabu baada ya kufanyiwa uchunguzi visivyo katika hospitali moja nchini.
Alisema alikutana na zaidi ya Wakenya 100 nchini India ambao pia walikuwa wathiriwa na wengine wao hali yao ilikuwa mbaya zaidi.
Alibuni mswada wa matibabu ambayo ana matumaini kuwa itakuwa sheria ili kuwawezaasha Wakenya kupata matibabu bora.