This archive report was first published on 11 September 2019.
Maafisa wa polisi walinaswa washukiwa wawili wanaoaminika kuhusika katika wizi wa magari katika maduka ya Thika Road Mall (TRM) na Garden City Jumanne, 11, 2019.
Washukiwa hao, Kelvin Mokaya na Moses Alimlim, walikuwa wakijaribu kukwepa katika vyumba vya kubadilisha nguo baada ya kuingia katika maeneo hayo kupiga tizi.
Maafisa wa polisi walipata ripoti kwamba washukiwa hao walikuwa wakiiba funguo za magari ya wateja na kutoweka nayo.
Maafisa wa polisi wanaamini kuwa washukiwa hao wamekuwa wakiwaibia wateja magari yao, vipakatalishi, simu, na bidhaa zinginezo katika maduka ya jumla ya TRM na Garden City Mall.
Washukiwa hao walinaswa kwenye kamera ya CCTV wakiwaibia wanunuzi waliokuwa wakitoa pesa kwenye mashine za ATM katika duka la Garden City Mall na Thika Road Mall.