This archive report was first published on 6 September 2019.
Msichana mmoja ambaye alijifungua mtoto msichana mwezi Juni mwaka huu, amemshtaki mwanablogu matata Dennis Itumbi kwa madai kuwa alimpachika mimba kisha akaingia mitini.
Alisema walikutana mwaka wa 2018 na penzi lao likashika moto, na baada ya hapo, Itumbi alikataa kukubali mimba ya binti huyo.
Msichana huyo anaitaka mahakama kumshurutisha Itumbi kuchukua jukumu la kulea ili mtoto wao apate malezi bora, na pia anataka nakala ya kitambulisho cha Itumbi ili aweze kumsajili mwana wao.
Alisema anataka pesa za matumizi ya kila mwezi, na kwa sasa anaomba msaada wa mahakama ili apate fedha za matumizi kutoka kwa mwanablogu huyo.
Itumbi ameshtakiwa kwa madai ya kukosa kutekeleza wajibu wake wa kulea baada ya kumpeana ujauzito na kutoroka.