Skip to main content

Seneta Cherargei: Raila anatumia Mau ili kummaliza kisiasa DP Ruto ▷ Kenya News

N

Nyakundi Report

Newsroom 1 min read

This archive report was first published on 5 September 2019.

Seneta wa Nandi Samson Cherargei amesema zoezi la kufurusha watu kutoka Mau ni mbinu yakummaliza kisiasa William Ruto. Picha: Nation

Alisema zoezi hilo limepangwa na Raila Odinga, na kuwa ni mbinu ya kisiasa kuhakikisha Naibu Rais William Ruto amemalizwa makali yake kufikia 2022 wakati wa mbio za kumrithi Rais Uhuru Kenyatta.

Cherargei alisema wapinzani wa Ruto walileta swala la wanasiasa kuchunguzwa maisha wanayoishi na kisha vita dhidi ya ufisadi.

Waziri wa Mazingira Keriako Tobiko alisema hakuna atakayesazwa kwenye zoezi la kuwafurusha watu kutoka msitu wa Mau.

Alisema serikali imejizatiti kuhifadhi msitu wa Mau na hakuna mtu atasazwa.

Alisema zaidi kuwa zaidi ya familia 10,000 zinatarajiwa kutolewa kwenye msitu wa Mau ikiwa ni zaidi ya watu alfu sitini.

Be the first to react

Support

Support this reporting

M-Pesa support recorded against this story.

Send support →

Stay close

Get the briefing

Major updates by email. No spam.

Get email brief →

Share

Save share card

Download a clean portrait card for sharing.

Save image →