This archive report was first published on 3 September 2019.
Kituo cha Habari cha Taifa Leo kinaeleza kwamba, jombi alikuwa amempeleka demu nyumbani na kumuhadaa mkewe alikuwa mfanyakazi mwenzake.
Alimwarifu mkewe kuwa alikuwa akiwatarajia marafiki zake na kumtuagiza awatayarishie kuku watakayekuja naye.
"Marafiki zangu tunaofanya nao kazi watakuja hapa kesho. Waliniarifu watakuja na kuku wapikie huku. Wote hawajaoa na wanatamani sana kula kuku wa kienyeji," jombi alimueleza mama.
Alisema hivyo wakati alikuwa akiwatarajia wageni wakati wa kula nyumbani.
Wageni waliwasili wakiwemo wanaume wawili na kispusa mmoja.
Walipowasili nyumbani humo, mama aliwapokea na kumchukua kuku waliyekuwa naye na kumchinja moja kwa moja.
Alipowasili kipusa alianza kumuuliza mama maswali ya kuchukiza.
"Mzee wako aliniambia bado hajapelaka mahari kwenu. Huo ni ukweli?" kidosho alimuuliza mama wa nyumba.
Alipomjibu kwa kuita kalameni ndani ya chumba cha kulala na kumuuliza nia ya mgeni wake, mkewe aliondoka chumbani humo na kuanza kumfokea kipusa huku akimfurusha jikoni mwake na kuku waliyekuja naye.