This archive report was first published on 22 August 2019.
Alisema hilo wakati alikuwa akizungumza na Lightharted akiwa na nyota wa NBA Josh Hart, wakati wa kujadili kuhusu kuondoka kwake klabuni na kuelekea Inter Milan.
Alisema kuwa alihisi kukataliwa na kutolindwa ugani Old Trafford kabla ya kukatiza mkataba wake na Manchester United.
"Mengi yamesemwa, lakini sikuhisi kulindwa nilihisi kama fununu nyingi zikienezwa, Rom anaweza kuondoka...hawamtaki Rom, na hakuna aliyejitokeza kuwakanya," alisema Lukaku.
Alisema kuwa aliondoka klabuni baada ya wiki nne za kujisubiri kwa mtu anayejitokeza kuwazima na kumlinda.
"Kwa wiki nne hivi nikisubiri angalau mtu ajitokeze kuwazima na haikuwezekana na nina jitambulia hivyo ndivyo itakavyokuwa," alisema.
Alisema kuwa aliamua kuchukua hatua kuhusiana na hatma yake baada ya fununu za uhamisho kuenea zaidi.
"Kwa hivyo nilijiwazia kwa wiki tatu na kisha nikayaona haya mambo yote kwenye mtandao jamii ni nani ambaye anafichua? Sio mimi wala ajenti wangu. Tunatazama tu kwenye simu yangu huku nikijiuliza ni nini haya?" alisema.
Alisema kuwa aliondoka klabuni kwa sababu alikataliwa na kutolindwa ugani na kuwa sio wajinga.