This archive report was first published on 27 July 2019.
Maafisa wa polisi wamewakamata wanawake wawili mtaani Kasarani na dola ghushi za kiasi kisichojulikana kwenye msako uliofanyika Ijumaa, Julai 27.
Wanawake hawa wawili, Catherine Wangechi Njanja na Yvonne Adhiambo Oduor, pia walipatikana na simu kadhaa za rununu.
Maafisa hao wametoa wito kwa wananchi ambao walipoteza mali yao kuzuru kitengo cha kupambana na uhalifu kilichoko makao makuu ya DCI, Kiambu ili kutambua bidhaa zao.
Washukiwa hao wanne, wakiwemo Joshua Murimi Ndegwa na Nelson Njoroge Wambui, walipatikana na vipakatalishi, simu, risasi na vifaa vya kompyuta kwenye duka hilo.
Washukiwa hao wanne watafikishwa mahakamani Jumatatu 29, Julai.
Source: Tuko.co.ke