This archive report was first published on 20 July 2019.
Julai 17, 2019, mwanamke wa Afrika Kusini alipokea nyumba mpya baada ya mchungaji kumfaa kwa nyumba nzuri ili aondokane na shida ya miaka mingi akiishi katika banda mfano wa chaka la simba.
Ingawa nyumba hiyo ingali katika hatua za kujengwa, mwanamke huyo anatazamia kuanza kuishi katika mazingira bora kuliko alivyokuwa akiishi.
Ufadhili wa nyumba hiyo ulikuwa wa kibinafsi kutoka kwa Mchungaji Eric Malulekena na Wasamaria wema.
Malulekena amesifiwa na kupongezwa kwa kuwa mfano mzuri unaotakiwa kuigwa na wachungaji wengine.
Ujumbe wa Tweet uliorushwa mtandaoni na Tonny Myambo ulielezea habari hii na kuonyesha picha za nyumba mpya.