This archive report was first published on 20 July 2019.
Binti ya Gavana wa Kiambu Ferdinand Waititu, Njeri Ndungu, alivalishana pete na Dkt. Nyotu Gitau katika harusi iliyofanyika Jumamosi, Julai 20, 2019, katika Kanisa la Presbyterian East Africa (PCEA), Runda.
Harusi hiyo ilizungumziwa sana Ijumaa, Julai 19, 2019, baada ya kuibuka kuwa, baba mkwe alikuwa ametengea kazi kubwa Bw. Harusi mtarajiwa katika serikali ya kaunti.
Harusi hiyo ilifanyika Jumamosi, Julai 20, 2019, katika Kanisa la Presbyterian East Africa (PCEA), Runda kisha makaribisho yakafanyika katika Hoteli ya Windsor Golf.
Waandishi wa habari waliona wanasiasa na wafanyabiashara maarufu akiwamo Ngina Kenyatta, mke wa mwanzilishi wa taifa Mzee Jomo Kenyatta, na mwanawe Muhoho Kenyatta, wakati wa harusi hiyo.
Bi. Njeri Ndungu, alivalia gauni lake maridadi huku Bw. Harusi akipiga pamba iliyoshonwa vizuri mtindo wa 'tuxedo'.
Hatimaye, makaribisho kemkem yalifanyika katika Windsor Golf Hotel and Country club ambayo Mamlaka ya Mazingira nchini (NEMA) ilikuwa anaelekea kuifunga baada ya kupatikana ikitupa maji taka katika mazingira.
Waandishi wa habari waliona wanasiasa na wafanyabiashara maarufu akiwamo Ngina Kenyatta, mke wa mwanzilishi wa taifa Mzee Jomo Kenyatta, na mwanawe Muhoho Kenyatta, wakati wa harusi hiyo.