This archive report was first published on 19 July 2019.
Julai 17, 2019, Kamishna wa Kaunti ya Bonde la Ufa George Natembeya alitoa wito kwa machifu wa Kaunti ya Elgeyo Marakwet kujitahidi zaidi katika kushughulikia ulemavu wa kijamii wa wezi wa mifugo eneo hilo.
Aliwataka machifu hao kuacha uzembe kazini ili kufanikiwa katika vita dhidi ya wezi wa mifugo, na kuwahimiza kukabiliana vikali na wahalifu ambao wamekuwa wakiwahangaisha wakazi wa eneo hilo kwa kuendeleza visa vya wizi wa mifugo.
Aliwashutumu maafisa hao hasa wa usalama wa Kaunti ya Elgeyo Marakwet kwa uzembe na kuwaonya kuhusu adhabu kali dhidi ya watakaokosa kutambua wezi wa mifugo.
"Haiwezekani kwa naibu chifu kutofahamu hawa watu ambao wamekuwa wakitembea na bunduki na kuwatisha wakazi wa hapa," alisema Natembeya.
Aliwaonya pia wahalifu na wezi wa mifugo kusalimisha silaha zao na kuwaonya kuwa serikali itatumia njia zinazofaa ikiwamo nguvu katika kutafuta bunduki zinazomilikiwa kinyume cha sheria.
"Nawaonya...tuthakikisha tunamaliza wizi wote wa mifugo. Tuko tayari kuwalipua kwa mabomu," alisema Natembeya.